Mtanzania Uganda
Ni nchi nzuri kwa kuishi na kufanya biashara. Nilifanikiwa kukaa Uganda kwa miaka mitatu na nikafanikiwa kutembelea baadhi ya sehemu kama Fort Porto, Mbarara, Lubirizi, Bushenti, Mbarara, Kasese, Igunga and Kabale. Hivyo nitaandika kutokana nay ale niliyo yaona au yasikia na kupata yaishi huko.
1. VISA:
Watanzania tunaruhisiwa kuingia na kutoka Uganda pasipo uwepo wa VISA ila
maranyingi ufikapo mpakani hupewa siku kulingana na shughuri inayo kupeleka
huko. Kwa wanafunzi huwa na nafasi zaidi zaidi ya hapo ni uwepo wa Shirikisho
la Mashariki ya Afrika.
2. Yellow
Card: Kutokana na kubadilisha hali ya hewa, Unatakiwa kuwa na Yellow Card
ambazo hutolewa katika hospitali za serikali, hii ni chanjo ambayo inatambulika
kimataifha na hudumu kwa miaka kumi kama sijakosea. Kwa Dar Es Salaam ni vyema
ukaenda mnazi mmoja utaipata haraka na pasipo usumbufu wowote.
3. Passport:
Popote pale passport au Hati ya kusafiria ni “Document”: Muhimu sana hivyo ni
vyema ukazihifadhi kwa umakini kwani vyaweza kukuingiza matatani. Na ni vyema
ukawa unatembea na kitambulisho chako hususani Passport kwani lolote laweza
kukukuta na kujikuta ukitakiwa onesha utambulisho wako.
4. Burudani:
Uganda inaburudani nyingi na kwa wanao ifahamu hifananisha Kampala na Los
Angels –Marekani. Ni vyema ukawa makini hapa kwani unaweza kujikuta unakula
mpaka nauli hakika. Pia kuna mitaa na madanguro ya madada poa ambapo napo
unatakiwa kuwa makini kwani wengine hutumia dawa za usingizi na kuishia
kukuibia kila kitu.
5. Usalama:
Ni jambo la kawaida kukaguliwa kila penye halaiki ya watu iwe ni kwenye ukumbi
au stendi hivyo ni vyema ukawa umejiandaa kwa ukaguzi nah ii yote ni kutokana
na hali inavyo badirika kwa uhalifu wa namna mbali mbali unavyo ongezeka kila
kukicha.
6. Lugha:
Kinatumika kingereza ingawa baadhi wanazungumza Kiswahili na lugha zao za
asili.
7. Kwa
wazazi na wanafunzi: Kama wewe ni mzazi lissome hili kwa umakini mkubwa.
Wanafunzi wa sekondari wanatabia hizi: Kujihamisha shule pale wanapo penda
wakifuata marafiki na unafuu wa ada ili waweze kuwa na pesa ya matumizi, wengi
hujihusisha na unywaji wa pombe na starehe za usiku, wengi hupenda kuishi nje
ya shule nikimaanisha kupanga mtaani.
Ufafanuzi:
Uganda kuna elimu nzuri tena sana, sifa imeharibika na wazazi wengi wanazidi
poteza imani juu ya kuwapeleka watoto wao kupata elimu Uganda. KOSA wafanyalo
wazazi ni hili, kuto kuwa na mawasiliano na walimu au shule husika, kuto fanya
risachi ya kutosha kuhusu shule umpelekayo mwanao na zaidi ni kumwamini mwanao
vya kutosha kwa kumwacha asafiri peke yake kwenda na kurudi,Ulipaji wa ada,
malazi njiani na mengineyo. Wengi huishi
katika vikundi na kutembea katika vikundi na kujikuta wakiishi bila kujifunza
chochote kipya.
8. Mavazi:
Mabinti huvaa mavazi mbali mbali na nguo fupi huvalika sana hususani jioni.
9. Ufugaji
wa nywele kwa wanaume: Wengi hawana mtizamo mzuri katika ufugaji wa nywele kwa
mwanaume namaanisha Afro pia kusuka nywele. Utasikia maneno kama Muyaye na
kadharika yakitumika yenye kumaanisha mtu mbabaishaji au asiye aminika kutokana
na mwonekano wan je wa haraka haraka.
10. Siasa:
Si vyema kujihusisha na mambo ya kisiasa na mamandamano kwani polisi hawana
msalia mtume katika hili.
11. Usafiri:
Kunausafiri wa aina tofauti kama Boda Boda –Usafiri wa haraka na wa hatari na Dala
dala ambapo wao huziita TAXI na tax za bongo kwao huitwa SPECIAL TAXI. Vituo
vya daladala huitwa stage na unapo taka kumsimamisha dereva ili akushushe sema
MASAO au STAGE. Kwa kawaida daladala zao hupakiza level seat na kulipa nauli
moja.
12. Vinywaji:
wanavinywaji kama Butunda, Kashera, Waragi na bia za dukani. Kuwa makini na
Waragi kwani kuna baadhi ni fake na zomesha sababisha madhara mengi kwa
watumiaji.
13. Sehemu
za kutembelea ukiwa huko: Munyonyo-Hoteli kubwa ya kitalii ambapo mikutano
mikubwa hufanyika, Gabba Beach, sehemu nzuri kwa kula samaki wakavu, Ukiwa
fortporto utaona Palace ya Mfalme wa kabila la Toro, pia ni mji ambao
inasemekana umejengeka vizuri, Namugongo - Sehemu walipo uwawa mashahidi wa
Uganda enzi hizo na kadharika.

No comments