Header Ads

Header ADS

Mtanzania Zimbabwe

Nilisha pata nafasi ya kutembelea Zimbabwe na kuweza zungumza na watu wachache na nilikaa kwa wiki moja na haya ndiyo niliyo yaona.
Zimbabwe ni nchi nzuri ingawa uchumi kiasi ni Tatizo. Yanayo andikwa kwenye vyombo vya habari hususani vyombo vya kimataifa na kufanya hata vile vya ndani kuandika kwa kuzingatia yanayo andikwa na kusemwa na vyombo vya magharibi mengi hayana ukweli sana.
1.       Tahadhari ukiwa zimbabwe: Uzoefu nilio upata kwa siku chache nilizo kaa Zimbabwe ni huu. Usipende kutembea tembea katika maeneo karibu na makazi ya raisi Mugabe, kama ni mtembea kwa miguu usipite maeneo hayo wakati wa giza na kwa mchana usipite upande barabara ilipo Ikulu yenye kumaanisha pita upande wa pili wa barabara.
Usitumie kamera maeneo hayo hasa kwa vitu kama kuji – Selfie au kupiga picha au video recording, Usipige makelele maeneo hayo.
2.       Matumizi ya pesa: Wanatumia dola kama pesa ya matumizi, kutokana na mzunguko wao dola ndogo ndogo zinachafuka sana. Hivyo unapo toka Zimbabwe hakikisha umepata dola safi kwani baadhi ya nchi huzikataa. Mfano nikiwa na dola nilizo zipata Zimbabwe iliniwia vigumu sana kubadirisha nikiwa Afrika Kusini mpaka ikanibidi nibadirishe kwa watu mtaani amnbapo ilikuwa ni hasara kubwa. Hili ni angalizo ingawa si la lazima sana.
3.       Lugha: Wazimbabwe wanalugha zao ila wanatumia kingereza kama lugha ya mawasiliano na wako – Polite pale uhitajipo msaada.
4.       VISA: Mtanzania anaruhusiwa kwenda Zimbabwe bila VISA na unaweza kuishi kwa miezi mitatu hii ni kwa mujibu wa makubaliano ya serikali yetu na yao hivyo hili laweza badirika muda wowote na saa yoyote, ni wajibu wako wewe kama mtanzania kuwasiliana na balozi zetu zahuko ili kuweza jua kama kuna mabadiriko katika hilo.
5.       Ubalozi: Ni vyema ukiwa Zimbabwe ufanye mawasiliano na ubalozi wetu kwani kunanyakati inasaidia sana hasa pale unapo pata dharura na hakuna mtu wa kumgeukia.
6.       Usafiri: Sijajua kama imebadilika ila na wao wana daladala kama sisi na wanaziita COMBI kama sijakosea na wakati sisi twaziita daladala. Ukiwa airport kwamfano unaweza angukia mikononi mwa walaghai wa mjini ambao wapo kila kona hivyo ni vyema kufanya mawasiliano na wenyeji wako mapema na kujua kiasi cha kulipa au kuwasiliana na hoteli kwa internet kabla hujaenda.
7.       Burudani: Kunakumbi nyingi za burudani ila nilifurahishwa zaidi na Book Cafee na msanii aliye nifurahisha ni Amara Brown na pia Vela the Plug.

No comments

Powered by Blogger.