Header Ads

Header ADS

Hasara iletwayo ni BIASHARA ZA NETWORKING. Mfano FOREVER LIVING, TIENS, EDMARK, GNLD Na nyinginezo.

Ni kwa-muda sasa biashara za mitandao zimekuwa zikipata nafasi katika masikio pia fikra za watu. Wengi wame loose concetration katika masomo pia usakaji wa pesa kwa njia madhubuti kama Kilimo na ufugaji na badala yake wamejikita katika biashara hii. Sisemi kama ni biashara mbaya, lahasha. ila najaribu itizama kwa mapana na marefu yake.

Biashara tajwa hapo juu zote zimejikita katika AFYA. Sekta muhimu na nyeti katika maisha ya mwanadamu natena katika mazungumzo yao au maelezo yao wanataja magonjwa mengi ila wanaweka msisitizo katika vitu kama Utoaji wa SUMU mwilini na kadharika. inafikia kipindi Dawa hizi zinauzwa mahospitalini kwa minajiri kwamba zinanguvu zaidi ya zile za hospitalini.

 Kibaya zaidi ni watu wanao toa elimu ya dawa hizi.
MOJA: Wamekaa kibiashara zaidi, asikudanganye mtu, watakuja na maneno kama tunajali afya yako na kadharika , ila ukweli ni huu... Wanacheza na Afya yako. muulize kiwango chake cha elimu, utaambiwa form two au form four na nikasomea Certificate ya Business administration. SWALI la kujiuliza: UMEONA kataja amesomea Medicine au afya ya mwanadamu? Ila akianza kukuhubiria kuhusu product zake utadhani ana PHD ya Baiolojia ya viumbe hai na viungo vyake hususani mwanadamu.

Mh! Acheni taaluma iitwe taaluma, na magumashi yaitwe magumashi. Unacho fanya wewe ni kumuongezea utajiri mwanzilishi huku ukipoteza muda wako na muda wa watoto wako, ambapo hawajikiti katika kufikiria mambo yenye maana na msingi na kujikuta wakipoteza muda katika haya mambo.

 Viingilio vyao: hapa pametofautiana, kuna makampuni yale ambayo yanachaji hela kubwa na yale yanayo hemea shingoni huchaji hela ndogo. Kinachotokea hapa ni hiki. wengi huingia mara baada ya kuhudhuria semina zao na kunogewa na maisha wanayo shuhudiwa kwamba nilikuwa meneja benki nikaacha na sasa nipo EDMAK, ninanyumba mbili, magari sita, ukiskia hivi nawe watamani. ulikuwa wapi miaka ya nyuma na kuwekeza pesa za mshahara wako katika vitu vinavyo dumu? Wengi tunashindwa kutofautisha kati ya ASSET na Liability. na hapa ndipo tatizo linapo kuja. Basi wakisha toa viingilio, hununua produkts kadhaa na hujaribu kuingiza wawili watatu, na mambo yakiwa magumu huacha na kurukia mtandao mwingine mpya. hiko nako hutoa kiingilio na kufanya yale yale. Usha wahi umepoteza shilingi kapi kama hivyo viingilio? hatukatai kujaribu kupo ili ufanikiwe ila hatuna buni kutumia mbongo zetu tunapo amua kujaribu.

KAMA WEWE UMEMALIZA CHUO KIKUU NA UNAFANI NA TENA HAUNA KAZI, Sikushangai. ila ukishindwa kufikiria mbinu nyingine za kujiajiri na badala yake ukaingia kwenye hizi biashara (Kumbuka umeingia huku baada ya kuwa fastreted na ushawishi na sio nafsi yako) basi nakupa ushauri wa - Kamwone daktari au mwanasaikolojia. Nakaribisha maoni na mitazamo yoyote, Lugha ni ruksa kutumia yoyote hata matusi ila kumbuka sheria isije kukubana, ukaishia kuwa victim.

No comments

Powered by Blogger.